| |
    
>>Kifo
Kisimani
>>Mwisho wa Kosa
>>Mayai Waziri...
>>Fasihi Simulizi
>>Maswali Ya Ziada


|
Chumba cha Majadiliano>>>
Tuma Maswali/majibu>>>
FASIHI SIMULIZI:
Hii ni sanaa itoayo maudhui yake kwa kutumia lugha ya maneno ambayo
hutamkwa au kutendwa.
Makala ya Fasihi Simulizi:
i)Lugha ndiyo itumiwayo fanani.
ii) Matumizi ya maneno kisanaa.
iii) Huonyesha hisia za binadamu.
iv) Hufunulia shughuli na kazi za watu husika.
v) Huonyesha uhusiano baina ya binadamu na mwingine.
vi) Humtazama binadamu na mazingira yake.
vii) Huwajenga watu kitabia.
Umuhimu wa Fasihi Simulizi:
i) Hutuwezesha kuelewa utamaduni na historia yetu vyema.
ii) Husaidia katika elimu ya jamii.
iii) Husaidia katika uga wa siasa- ulumbi
iv) Hukuza ufasaha na ustadi wa mtambaji.
v) Hufurahisha na kuburudisha.
vi) Huendeleza umoja na utangamano.
vii) Hukuza mtalaa wa lugha.
viii) Huipa jamii mwelekeo na nasaha kwa kuonya na kushauri.
ix) Hukuza upeo wa wanafunzi.
x) Hufunza mbinu za sanaa na uchambuzi.
xi) Kupokezana utamaduni wa jamii.
xii) Kukuza maadili katika jamii.
xiii) Ni kazi kwani watu hupata malipo kutokana na fasihi.
xiv) Huwazindua watu ili wajue haki zao.
xv) Hurekebisha tabia.
Sifa bainifu za uwasilishaji wa Fasihi Simulizi na Fasihi Andishi:
Fasihi Simulizi
Fasihi Andishi
1. Huwasilishwa kwa mdomo
-Hutegemea maandishi yasomwayo
2. Hadhira huwasiliana na mwasilishaji
-Si lazima hadhira iwasiliane na msimulizi
3. Hadhira huweza kuchangia
-Hadhira haina njia ya kuchangia usimulizi
4. Humilikiwa na jamii
-Ni milki ya mtunzi au mwandishi
5. Ina tanzu nyingi
-Haina tanzu nyingi
6. Sifa zisizo za lugha kutumika
-Hutegemea sifa za lugha isipokuwa igizo
7. Huonyesha ubunifu mpya
-Hubakia kama ilivyoandikwa na mtunzi
8. Huifadhiwa akilini kwa kukumbuka
-Huifadhiwa kwa maandishi vitabuni
9. Huweza kubadilishwa (ufaraguzi)
-Msomaji hana uhuru wa kubadilisha
10. Msamiati wa utungo kupotea
-Kazi hubakia kama ilivoandikwa
11. Kuambatanisha na utendaji
-Haiambatanishwi na utendaji ijapo’ igizo
12. Hutumia wahusika changamano
-Hutegemea sana wahusika binadamu
Muainisho wa Fasihi Simulizi:
Tanzu nne kuu za Fasihi Simulizi ni:
a) Hadithi/ Simulizi-hutumia lugha nathari
b) Maigizo-uwasilishaji mbele ya hadhira
c) Semi- ufupi wa kimuundo
d) Ushairi- uimbaji na muundo maalum
Vipera vya Tanzu hizi:
a) Hadithi/ Simulizi
b) Maigizo
i) Migani/ mighani
I) Michezo ya jukwaani
ii) Hekaya
ii) Mazungumzo
iii) Khurafa/ hurafa
iii) Vichekesho
iv) Ngano za mazimwi
iv) Ngomezi
v) Soga
v) Ulumbi
vi) Ngano za mtanziko
iv) Malumbano ya utani
c) Ushairi
d) Semi/ Tanzu-bainifu
i) Nyimbo
I) Methali
ii) Ngonjera
ii) Nahau
iii) Sifo
iii) Misimu
iv) Maghani
iv) Misemo
v) Majigambo
v) Lakabu
vi) Vitendawili
vii) Vitanza-ndimi
Katika ukurasa ufuatao tunaangazia mengi kuhusu
ngano.
<<Ukurasa wa Kwanza
Ukurasa Ufuatao>>
|
|